Friday 23 May 2014

Roho ya msamaha ni msingi wa kwenda mbinguni.

Tunapo kuwa tumemwamini Yesu kuwa Bwana na mwokozi wetu, tunakuwa tumetangaza vita na ufalme wa shetani. Hivyo wengi sana shetani atawafanya watufanyie makosa ya makusudi tu, je tuwachukie? Hapana. Tuwapende na kuwaombea, Mfano Yesu Kristo hakupendwa na wote japo alikuwa akifanya mema kwa watu, aliponya wagonjwa, kufufua wafu, vipofu kuona lakini bado walifanyia mabaya mpaka kmwua msalabani. Jambo la ajabu ambalo Yesu alifanya ni kwamba aliwaombea msamaha wote waliomtendea mabaya. Katika Lk 23:34.  Na umhimu wa kusamehe Yesu ali ufundisha sana kwa wanafunzi wake katika Mt 6:24 na ndiyo maana mitume nao waliwafundisha wengine maana tunaona matokeo ya mafundisho yao kwa Stefano alipopigwa mawe kwa sababu ya kuhubiri kabla haja kata roho naye aliomba msamaha kwa wale waliomfanyia kitendo hicho. Mdo7:59-60.

Kwa nini tusahehe, ni kwa sababu sote tumekosa na ili Mungu asamehe makosa yetu ni lazima tuwasamehe wengine makosa yao. Mt 6:24

Nimalize kwa kusema samehe wengine ili ujiwekee akiba ya kumfanya Mungu akusamehe wewe. Na huo ndio mlango wa wewe kuziona baraka za Bwana. Amen!!!

No comments:

Post a Comment