Wednesday 28 May 2014

Umezaliwa ili ukue katika Kristo Yesu.

Mara tu baada ya kumwamini Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yetu, huwa tumezaliwa katika ufalme wa Mungu. Yohana 1:12. Tunakuwa hatujui mambo mengi kiroho yaani ni kama mtoto mchanga kimwili asivyoelewa maisha ya kimwili. Neno la Mungu linatueleza, Lakini Kueni katika neema na katika kumjua Bwana wetu na mwokozi Yesu kristo. 2 Petro 3:18.

Hatua mhimu za kufanya ili tukue kiroho.
(1) Lazima tupende mafundisho ya neno la Mungu. 1Petro 2:2, Ebrania 5:12-14.
(2) Tuwa epuke marafiki wasiomcha Mungu. 2Kor 6:14-18
(3) Tuwe watu wa maombi Wafilipi 4:6-7
(4) Tutii neno la Mungu.

Anza kwa kufanya hayo kwanza na Mungu atabadilisha maisha yako.
Ubarikiwe sana!!! Amen

No comments:

Post a Comment