Tuesday 10 June 2014

Kwa Neema ya Bwana Nimepanda kanisa jipya tena.

Wafilipi 4:13
Ninayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu. Kwa wiki tatu sasa ni Mungu ameniwezesha kupanda kanisa jipya katika kijiji cha Kasuguti, kata ya Kasuguti, Tarafa ya Kikombwo wilayani Bunda mkoa wa Mara. Kabla ya kwenda kupanda kanisa hili, nilisikia sauti ndani ya moyo wangu ikiniambia kwenda kuanzisha kazi mpya. Kwa hiyo niliamua kuitii sauti hiyo.

Kwa hatua ya mwanzo niliamua kwenda kumwona mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kasuguti ili kunipa chumba cha darasa kwa ajili ya kukusanyikia humo maana ndio utamaduni wetu katika hali ya mwanzo ya kuanza kanisa jipya maeneo haya. Ninamshukru Mungu Kwa moyo mzuri niliouona kutoka kwa mwalimu huyo, yeye aliniruhusu akasema hawezi kukataa kuruhusu kazi ya Mungu kuanzishwa katika eneo hilo. Hivyo nilianza kupita nyumba hadi nyumba nikiwashuhudia habari za Yesu Kristo.

Kila niliye kutana naye nilimweleza habari za Yesu na wapi tunapatikana kwa ibada. Ibada yangu ya Jpili ya kwanza niliabudu na watu wazima watatu na mtoto mmoja, siku ya Jtano akaongezeke mmoja, na Jpili ya ya tar 8June nikaabuda na watu wazima Tisa na watoto sita. Kweli nimelihakikisha neno la Bwana Yesu aliposema Mavuno ni mengi ila watenda kazi ni wachache na kwamba tumwombe Baba wa mavuno apeleke wavunaji. Ni kweli!!!!

Ndugu mpendwa katika Bwana, ninaomba maombi yako ili Mungu aiinue kazi yake zaidi. Kumbuka Shetani hutamani zaidi kuua hasa kwa kitu kilicho kichanga bado. Wakati Musa alipozaliwa alitafutwa na Farao ili auawe, Yesu alipozaliwa naye alitafutwa na Herode ili auawe na badala yake watoto wengi wakachinjwa. Nk Tuombee ili kufikia maono hapo chini.

Maono yangu kwa kazi hii, Mwaka huu ninatamani nipate pesa kwa ajili ya kununua kiwanja cha kanisa, ikiwezekana tulete mawe, mchanga na tuujenge.  Hagai1:8

Ubarikiwe na Bwana,

No comments:

Post a Comment