Saturday 13 September 2014

Pongenzi kwa askofu Batenzi.

Ninapenda kuchukua nafasi hii Kumshukru sana Mungu kwa ajili ya uongozi mpya wa kitaifa kanisa la Free Pentecostal Church Tanzania (FPCT) uliopatikana leo jioni baada ya kufanyika uchaguzi halali katika bwalo la UDOM Dodoma. Halmashauri kuu ya kanisa taifa, kwa pamoja tumekuwa UDOM toka 9/92014 tukiendelea na semina yenye baraka nyingi sana. Askofu toka Sudani ya Kusini Ngd Daniel amefundisha neno lililokuwa na lengo la kuwafanya watumishi wa Mungu wayaige maisha ya Yusufu mtoto wa Yakobo kwa jinsi alivyokuwa mwaminifu toka kwa familia ya baba yake, nyumba ya Botifa, gerezani na misri pia. Kutikana na neno la Mungu linaonyesha kuwa pote alipo pita Yusufu alikuwa akimwinua Mungu wake.

Hitimisho la semina hii ni uchaguzi wa uongozi wa kitaifa, Hongera David Batenzi kwa kuchaguliwa tena na Mungu ili uweze kuiongoza FPCT kwa miaka mitano. Mungu ana kusudi na wewe, angalia Mungu amekuchagua kuwa mwenyekiti wa CPCT, tena UKIAMKA, Ubarikiwe sana. Hongera Katibu mkuu Elias Shija kwa kuchaguliwa tena. Na wengineo.  Mungu awabariki sana.





No comments:

Post a Comment