Saturday 15 November 2014

UMHIMU WA MAOMBI KWA MKRISTO WA LEO.

Maombi na umhimu wake mbele za Mungu:

Mungu ameweka ujumbe huu ndani ya moyo wangu na ninaomba nikushirikishe ili uweze kupokea baraka tele zilizomo ndani ya ujumbe huu. Ili uweze kuelewa ni lazima sasa nieleze nini maana ya maombi.
(1) Maombi ni mazungumzo baina ya mtu na Mungu au Mungu na mtu aombaye kwake. Isaya 1;18. Mungu anaongea hapa na akionyesha pia matokeo yake kwa mwombaji ambaye amekubali kwenda mbele za Mungu katika hali ya kusemezana naye.
 (2) Maombi ni kumwita Mungu juu ya shida au tatizo lolote ulilonalo, ukihitaji msaada wa jambo hilo. Yer 33;3.
 (3) Maombi ni kutafuta ufumbuzi katika Mungu juu ya kile unachotaka kuona Mungu anahuska nacho.2Nya7;14, Mt 7;7. Kuna lugha nyingi sana zilizotumika katika Biblia zinazoonyesha maombi kwa maana hizi.
 Kwa kila mwammini mara tu baada ya kuokoka anapaswa kuanza na kujizoeza kuomba kwani ni mhimu sana katika ukuaji wa maisha ya kiroho na ndiyo maana nikichukua mfano kwa mitume, watu waliotembea na Yesu alipokuwa katika mwili, mara tu  alipowaacha waliendelea kukumbuka kile ambacho Yesu alikifundisha na wakaanza kutii na kufanya, Mdo 2;42. Katika Efe6;10-19. Maombi yametanjwa kuwa ni silaha kwa mwamini, kuomba au kusali (maana ni ile ile) ni sharti kuu na jambo la kujumlisha maisha ya imani na ushuhuda wenye matunda kwa mtoto wa Mungu.

Kweli pasipo kuomba maisha ya hapa duniani ni bure kabisa. kuomba ni njia pekee ya kutuunganisha na chemichemi za uzima wa kweli, yaani na Mungu. Wakati wowote maungamo haya yapo, uzima huu wa Mungu unatujia. Maungamo hayo yakiharibika, matokeo ya lazima ni kwamba, mto huu wa kutuletea maji ya uzima na nguvu unakauka. Na hivyo mtu wa ndani aliyetoka kwa Mungu hurudi nyuma na kunyauka pole pole na kushidwa kukua kiroho kabisa.

Kwa sababu hii, tungeweza kudhani kwamba mtu awezaye kuomba sawa sawa, ni yule tu ambaye amekwisha kuunganishwa na chemichemi ya nguvu hiyo, amekwisha kuwa mtoto wa Mungu. Lakini Biblia inaonyesha kwamba hata mtu ambaye hajazaliwa mara ya pili, lakini anamcha Mungu anaweza kumkaribia Mungu kwa njia ya maombi na kwamba Mungu anaweza kusikiliza maombi yake na kuyajibu pia. Lk 18;13-14, Mdo 10;1-4. kujibiwa kwa maombi si thibitisho la kuwa mtoto wa Mungu, bali ni thibitisho la kuwa mchaji wa Mungu tu. Yeye amtafutaye Mungu kwa njia ya kweli ataanza kwa kuomba na kusoma neno lake. Kwa kufanya hayo uhusiano na Mungu huanzishwa na unahitajika kutunzwa.

Maandiko yana tuhimiza kuchunguza jambo hili la maana sana kwa kujiuliza maswali manne:-
                                       (1) Kwa nini kuomba.
                                       (2) Jinsi gani kuomba.
                                       (3) Wakati gani kuomba.
                                       (4) Kwa kusudi gani kuomba.
-; (1) Kwa nini kuomba,
          (a) Mwili ni dhaifu Mt 26;41; kwa maneno haya Bwana mwenyewe alitoa sababu na jibu la swali letu. Dhiki na taabu hufundisha kuomba Zab 50;15. Katika kuomba tunatambua dhiki na kutokuweza kwetu zaidi. Kwa hiyo mara nyingi Mungu mwenyewe anakubali mtu apate dhiki ili amwonyeshe udhaifu wake na kumkumbusha kwamba msaada wa kweli uko kwake. Ayu.33;30,26

Kama Bwana wetu Yesu mwenyewe,  katika siku za mwili wake, alitoa maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi.................... ingawa ni mwana .............. Ebr. 5;7  si zaidi sana sisi tunahitaji na kutegemea hayo!
          (b) kwa sababu adui ana nguvu na vita ni vikali.
Ni mhimu kuelewa kwamba tunashindana na adui mwenye nguvu kuliko mwanadamu wa kawaida ( asiye na nguvu ya Mungu ndani yake) Kwa hiyo kushinda naye kwa nguvu zetu za kawaida ni bure kabisa.  Zaidi ya hayo kushindana naye na kushinda tunaweza kwa njia ya imani tu. ( Imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la Kristo, Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo bayana ya mambo yasiyoonekana Warumi 10;17, Ebr11;1). Lakini imani hai ni kuunganika na  Mungu kabisa. Kuunganika kwetu na Mungu kunatunzwa kwa njia ya maombi tu.  1Petro 5;8-9, Flp 4;6-7 Kwa sababu hiyo mtume Paul alijumulisha silaha zote kwa vitavkuu ya kutisha katika silaha kubwa inayotajwa mwishoni ....... katika sala, baada ya kuonyesha nguvu ya adui yetu itishayo kwa mwanadamu. Efe, 6;11-12, 13-17,18!!! 

Ushindi mkubwa kabisa katika historia yote na mashindi makubwa mengine yote, hayakupatikana kwa mapanga na baruti bali yalipatikana kwa kukaa magotini (maombi) Mdo12;1-4 (Mateso ya kanisa) Mst 5, Kanisa liliomba kwa nguvu. Mst 6-17 Majibu na matokeo ya maombi kwa kanisa. 

Yawezekana huduma yako, iko gerezani, ndoa yako iko gerezani, masomo yako, yako gerezani, ajira yako iko gerezani, biashara yako, iko gerezani, NK. Fanya kama kanisa lilivyofanya, shirikisha Mchungaji wako, nk ili kuomba pamoja na ninaamini gereza hilo litafunguka katika jina la Yesu Kristo!! Usiogope Bwana yuko pamoja na wewe.
        (c) Kwa sababu Mungu ana hamu ya kusikia sala na maombi ya watoto wake, ana wahimiza kufanya hivyo mara mara. (Zab50;15, Mt 7;7, 2Nyak 16;9, Yn 4;23b!) Zaidi ya hayo Mungu anaziheshimu sala namna hii hata azitie katika vyombo vya dhahabu na kuzipokea pamoja na mziki. Ufu 5;8. 

Maendeleo na matokeo makubwa mbinguni na duniani, Mungu ameyaweka yategemee maombi na sala za watoto wake. (1Fal 18;36-39, 2Fal 6;17, Dan Sura 9-10, Yak5;16-18, Ufu 8;3-8)   
                              Kumbuka   maendeleo makubwa haya yanategemeana.



Ubarikiwe sana kwa kutembelea Blog hii na endelea ili upate mafundisho Kutoka kwa mch Philip Buluba aliye na mzigo wa kupanda makanisa maeneo yasiyo fikiwa na injili hapa Tanzania. Somo hili linaendelea...

No comments:

Post a Comment